
Kwa kweli nina hasira, kwa yale unayotenda
Wewe ulo na ajira, mesahau ya kalenda
Wanipa chache mshara, uso fika siku kenda
Nimechoka na kuimba, nilipe na nitaenda
Mwezi umekamilika, hadi lini tasubiri?
Mwajiri waajibika, waniumiza kisiri
Hu ni ukweli hakika, moyoni waniathiri
Nimechoka na kuimba, nilipe na nitaenda
Nazivunja zangu sera, nizokuwa nimetenga
Nipe wangu mshahara, labda jumba tajenga
Nikuwapo na subira, waniona mi mjinga
Nimechoka na kuimba, nilipe na nitaenda
Wewe wacha zako pupa!, hivyo ndo waniambia
Njoo kesho nitakupa, na kikomo ushatia
Nijapo kile wanipa, nashindwa kukipangia
Nimechoka na kuimba, nilipe na nitaenda
Kazi hi nipo chagua, lijua tavumilia
Ila yanayotokea, naona kujiondoa
Mwajiri nakulilia, haki zangu natetea
Nimechoka na kuimba, nilipe na nitaenda
Mbona sasa wanyamaza?, kilio changu sikia
Haki zangu nauliza, mbona kazitupilia
Kwako wewe wala piza, nami nja navumilia
Nimechoka na kuimba, nilipe na nitaenda
Fuata zote sheria, zotengwa na serikali
Mwajiri u zingatia, haki zangu za awali
Maskini naumia, mana uchumi u ni ghali
Nimechoka na kuimba, nilipe na nitaenda.
@jephinternational
Jeph Internationalさんをフォローして最新の投稿をチェックしよう!
0 件のコメント
この投稿にコメントしよう!
この投稿にはまだコメントがありません。
ぜひあなたの声を聞かせてください。